TANZANIA KUENDELEZA DHAMIRA YA KUFIKIA AGENDA 2063

Font size:

Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango, amesema Tanzania inaendelea na dhamira yake ya kushiriki katika kutekeleza Ajenda ya Maendeleo ya Afrika 2063, kupitia uwekezaji wa kimkakati katika sekta mbalimbali kama vile miundombinu ya usafirishaji, nishati, kilimo, viwanda, TEHAMA, uhifadhi wa mazingira na maendeleo ya rasilimali watu.


Dkt. Mpango amesema hayo alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Mkutano wa 42 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Bodi ya Juu ya Shirika la Maendeleo la Umoja wa Afrika (AUDA - NEPAD), uliyofanyika kwa njia ya Mtandao na kuongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo ambaye ni Rais wa Misri Abdel Al Fattah El - Sisi.


Kadhalika Makamu wa Rais amesema, ni muhimu nchi za Afrika kuimarisha vyanzo vya mapato vya ndani, kwa kutumia vyema rasilimali za nchi kama vile madini pamoja na kushirikiana na sekta binafsi ili kukabiliana na upungufu wa fedha za ufadhili wa miradi katika kutekeleza Ajenda 2063.

 

or

For faster login or register use your social account.

Connect with Facebook